DHANA MUHIMU (KEY CONCEPT) – Swahili

DHANA MUHIMU (KEY CONCEPT)

 Uthamini wa Forodha  (Customs valuation)

Uthamini wa Forodha ni mchakato wa kuamua thamani ya bidhaa ambazo zimeagizwa/zimeletwa nchini ili kutozwa kodi.

 Thamani ya Forodha

 Hii ni thamani ya bidhaa ambazo zimeagizwa/zimeletwa nchini ili kutozwa kodi/kuhesabu kodi ya Forodha (Customs ) ya ad valoremi na kodi zingine.

  • Kwa bidhaa ambazo zimeagizwa kwa njia ya reli na kwa usafirishaji wa maji, thamani ya Forodha itakua kwa jumla la bei yenyewe ambayo imelipwa, ambayo inafaa kulipwa kwa bidhaa, gharama ya bima na mzigo (insurance and freight).
  • Bidhaa ambazo zimeagizwa kwa njia ya usafirishaji wa angani (air transport ) thamani ya Forodha itakua kwa jumla la bei yenyewe ambayo imelipwa, bei ambayo inafaa kulipwa kwa bidhaa na gharama ya bima na ya mzigo. Mzigo (freight)  haiwekwi kwa bidhaa ambazo zimeagizwa nchini kwa njia ya usafirishaji wa angani.

 Kodi ya ad voleremi

 Hii ni kodi ambayo inawekwa kwa thamani ya bidhaa na kwa kawaida huwekwa kwa asilimia ya thamani ya bidhaa (commisssion). Kodi hizi ni tafauti kwa kodi fulani ya kuwekwa kwa kiwango ya  idadi fulani  (specific duty/measures). Hukuwa kwa idadi kama nambari, uzito, wingi, eneo/upana na kwa uwezo, baadhi za zingine.

 Kuna uwezekano wa kukuwa na kodi ya kutozwa ya mchanganyiko (composite) ambayo kwa kiasi ni ya ad valoremi na kiasi cha idadi fulani  (specific measures) kama kwa manguo 3.5 kwa kila kilo au 35% ile ambayo ni nyingi ndio itachukuliwa. Tarifi/kodi ya Forodha (Customs )  ya Uganda ambayo inawekwa kwa kila bidhaa, inachapishwa kwa kila Gazeti ya Uganda kila mwaka wa fedha.

AINA ZA KUPIMA THAMANI ZA FORODHA (CUSTOMS VALUATION)

 Kuna aina sita za Kimataifa za kupima thamani za Forodha  (Customs ) kwa bidhaa ambazo zinaletwa nchini ambazo zimeletwa kwa Makubaliano ya Shirika ya Biashara ya Dunia (WTO) kwa Makubaliano ya kupima Thamani. Aina hii inafuata mlolongo/amri ya mlolongo (sequence).

 Aina ya Msingi ya kupima thamani ni aina ya kupima thamani ya shughuli (transaction value method), ambayo ni bei yenyewe ambayo imelipwa, inafaa kulipwa kwa bidhaa ya mauzo nje ya nchi hadi nchi ya uagizaji/kwa nchi ambayo inaingiza bidhaa. Masharti fulani ya idadi ya lazima itimizwe/iwekwe ili kutumia aina ya thamani ya shughuli (transanction value method) na inaweza kukuwa na aina ya kuongeza au kupunguza kama malipo ya asilimia (Commission) au royalti.

 Kama shughuli ya kupima thamani haiwezwi kutumika, aina moja kwa zingine itatumika kuamua thamani ya Forodha (aina ya kupima thamani) kwaamri ya mlolongo (order of sequency)

 

  • Aina ya shughuli ya thamani ya bidhaa ambazo zinafanana kamili/kipacha (identical goods) – Hizi zinatumia shughuli za thamani za bidhaa ambazo zinafanana kamili/kipacha ambazo ziliyofanyiwa kliarensi/kibali cha Forodha (Customs). Bidhaa ambazo zinafanana kamili/kipacha ni bidhaa ambazo zinafanaa kwa aina zote isipokuwa tafauti madogo kama rangi au ukubwa. Bidhaa zinafaa kukuwa za chapa (brand) zinazofanana na zinatoka kwa nchi moja ya mauzo nje (country of export).
  • Thamani ya shughuli, aina ya thamani ya bidhaa ambazo zinafanana (value of a similar goods) – Hii inaamua thamani ya shughuli za bidhaa ambazo zinafanana, bidhaa ambazo zilifanyiwa kliarensi zikivukishwa kwa Forodha (Customs ). Bidhaa ambazo zinafanana kisifa (characteristics) na zinawezekana kutumika kwa niaba ya ingine kifedha; kama mteja hawezi kupata bidhaa imbazo zinafanana kamili wanaweza kuchukua zingine za matumizi ambazo zinafanana kama (Colgate na Close up). Kama bidhaa zinafaa kuchukuliwa ati zinafanana ki-chapa (brand) zinafaa kukuwa na sifa (reputation) kama LG na Samsung; na zinatoka kwa nchi ya uasili moja.
  • Aina ya kupunguza thamani – Msingi wa thamani ya Forodha (Customs ) ni bei ya kwa jumla za idadi za bidhaa ambazo zimeletwa nchini, zinauuzwa Uganda. Gharama na kodi baada ya uagizaji/kuleta bidhaa nchini zinapunguzwa ili kufika kwa thamani ya Forodha  (Customs).

 Gharama ambazo zinapunguzwa ni

  • Kodi kama VATI, Kodi ya Uagizaji (import duty), Kodi ya Madhara (Excise duty).
  • Faida na gharama zote kama nauli/kodi ya nyumba,

○ Faida na gharama zote kama nauli/Kodi ya nyumba, kazi nakadhalika ambazo zinahusika na usambazaji na mauzo za bidhaa .

 ○ Gharama baada ya uagizaji /kuleta bidhaa nchini ambazo zinahusika na usafirishaji wa bidhaa hadi ghala ambayo iko na bondi  (bonded warehouse).

  • Aina ya thamani ya jumla/iliyohesabiwa (Computed value method) – Msingi wa gharama  ya uzalishaji (producing ) wa bidhaa kama malighafi (raw material) vitu vya kutumia na gharama zote kwa jumla, gharama zingine na faida ambazo zinahusiana na uzalishaji  (production) na mauzo za bidhaa ambazo zimeagizwa nchini. Aina hii inafaa kupata habari kutoka kwa nchi ya uzalishaji (production).
  • Kushuka kwa thamani (fall back value) kama hakuna aina zingine ambazo ni sawa, ya msingi ya thamani ya Forodha (Customs) inaweza kuwekwa kwa moja kati ya aina tano halafu marekebisho inafaa  kufanywa ya kupunguza/kuongeza. Aina hii haitumiki kipekee na inafaa kutumika ikitegemea mlolongo (sequence) ya kutafsiri rahisi (flexible interpretation) ya aina kutoka kwa 1 hadi 5 hadi thamani ya bidhaa kuamuliwa.

Forodha (Customs) itaamua thamani kwa kutoa uamuzi kutoka kwa habari ambazo zimepeyana hapo juu na habari zingine ambazo zinafaa.

 MCHANGANYIKO WA THAMANI WA FORODHA (COMPOSITION OF CUSTOMS VALUE)

Thamani ya Forodha zitakuwemu zifuatavyo;

  • Gharama ya bidhaa ya bure ambayo imewekwa kwa chombo/meli/ndenge kwa nchi ya mauzo ya nje (exporting country).
  • Malipo ya mizigo/ gharama ya mizigo hadi pahali pa uagizaji kama bidhaa zitasafirishwa kwa reli au bahari.
  • Upakiaji,ushukishaji, na gharama zingine ambazo zinahusiana na usafirishaji wa bidhaa hadi pahali pa uagizaji/uletaji bidhaa nchini;
  • Na gharama ya bima (insurance )

 Ukaguzi wa mizigo kabla ya usafirishaji (Pre-Shipment Inspection).

 Gharama ya ukaguzi wa kawaida kabla ya usafirishaji inalipwa na muagizaji (importer) au Serikali la nchi ya uagizaji. Ukaguzi hizo zinaweza kufanywa kulingana na sheria la nchi ya uagizaji, kulingana na mahitaji ya Shirika la kutoa usaidizi/msaada wa fedha/bidhaa kama mahitaji ya Shirika la kutoa usaidizi. Gharama ya ukaguzi kabla ya usafirishaji sio miongoni ya thamani ya Forodha  (Customs value).

Jumla la gharama ya thamani ya Forodha.

Sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Udhabiti wa Forodha (EACCMA) inahitajika ati idadi ya gharama zingine na thamani ya bidhaa zingine na huduma kama haijawekwa kwa bei ambayo imelipwa au ambayo inafaa kulipwa kwa bidhaa ambazo zimeagizwa nchini/zimeletwa nchini lazima ziongezwe kwa bei ambayo imelipwa au inafaa kulipwa, gharama  na thamani itakuwemu idadi zifuatavyo

  • Malipo ya asilimia (Commission) na ya dalali/broka isipokuwa malipo ya asilimia ya ununuzi (buying commission)
  • Gharama ya chombo/kontena
  • Gharama ya kupakia (packing)
  • Usaidizi (assists) (bidhaa na huduma ambayo mnunuzi amempa muuzaji bila malipo au kwa bei iliyopunguzwa ili kutumia kwa uzalishaji (production) wa bidhaa ambazo zimeagizwa/zimeletwa nchini.
  • Royalti na nauli ya leseni
  • Faida zinazofuatana na (mazuri za kifedha kutoka kwa kuuza tena au kutumia bidhaa ambazo zimeagizwa na mnunuzi).
  • Gharama ya usafirishaji na bima hadi pahali pa usafirishaji wa moja kwa moja hadi nchi mkazi (partner state.)

 Gharama ya kupakia  (packing costs)

 Gharama ya ufungaji/kupakia (parkings) nje ya nchi (overseas) pamoja na nyenzo (material) na kazi inawekwa pamoja kwa thamani ya Forodha ya bidhaa. Gharama ya chombo/kontena na paleti ambayo imeagizwa/imeletwa nchini haiwekwi pamoja na thamani ya Forodha.

 Thamani ya Forodha iko kwa sarafu (currency) ambayo imekubaliwa kwa ankara ya biashara (commercial invoice). Kwa hayo kwa kusudi (purpose) ya kulipa kodi na Ankara (invoice) iko kwa fedha ya Kigeni. Thamani ya Forodha inabadilishwa kwa shilingi ya Uganda, kwa kutumia cheo ambacho kinachapishwa kila mwezi na Shirika la Mamlaka ya Mapato Uganda.

KUHESABU KODI YA UAGIZAJI (IMPORT DUTY)

Hatua 1

 Amua thamani ya Forodha ya kifaa (item), hii ni jumla ya malipo, bima na mzigo hadi bandari (port) ya uagizaji/kuleta bidhaa hadi EAC kama Mombasa, Der es Salaam.

Hatua 11

 Badilisha fedha kwa shilingi ya Uganda kwa kupigisha thamani ya Forodha na cheo ambacho iko.

 Hatua 111

 Amua (determine) kodi ambayo inafaa

 Kwa mfano

Kama umeleta gari ambayo ni mzei kuliko miaka 9 kwa bei ya FOB USD 2000, umelipa USD 200 kwa bima (insurance) na USD 300 kwa gharama/malipo ya mzigo hadi Mombasa na cheo cha kubadilisha fedha ni USD 1= shilingi 3,600.

 Hatua 1

 Thamani ya forodha = Gharama + Bima + Mzigo.

 =Gharama + Bima + Mzigo

 = 2000 + 200 + 300

 = 2500

 

 

 Hatua 11

Thamani ya Forodha = Thamani ya Forodha x Cheo/kiwango cha Ubadilishaji fedha

 = 2500 × 3600

 = 9,000,000

 Hatua 111

 Amua (determine) kodi

 Kodi ya uagizaji = 25%, VATI= 18%, Kodi ya Kubakishwa = 6%, Kodi ya Mazingira = 50% (kama uzei wa gari inazidi miaka 9 kutoka kwa wakati iliyotengenezwa), Kodi ya kutumia vifaa kama barabara = 1.5%.

 Hesabu

Kodi ya Uagizaji (Import duty)

 = 25% × 6,250,000

 = 25/100 × 9,000,000

 = 25/100 × 9,000,000

 = 2,250,000

VATI

 = 18% ya (Thamani ya Forodha + Kodi ya Uagizaji)

 = 18% ya (9,000,000 + Kodi ya Uagizaji)

 = 18% × (9,000,000 + 2,250,000)

 = 18/100 × 11,250,000

 = 2,025,000

Kodi ya Kubakisha (WHT)

= 6% ya thamani ya forodha

= 6% × 9,000,000

 = 6/100 × 9,000,000

 = 540,000

KODI YA MAZINGIRA

 = 50% ya thamani ya forodha

 = 50% × 9,000,000

= 50/100 × 9,000,000

 = 4,500,000

 

 KODI YA MIUNDOMBINU (INFRASTRUCTURE)

 = 1.5% ya Thamani ya Forodha

 = 1.5% × 9,000,000

 = 135,000

 KODI KWA JUMLA/JUMUISHA (SUM)

 = Kodi ya Uagizaji (Import duty) + VATI + Kodi ya Kubakishwa  (WHT) + Kodi ya miundombinu/vifaa + Kodi ya Mazingira

 = 2,250,000 + 2,025,000 + 540,000 + 135,000 + 4,500,000

 = 9,450,000

KUPIMA THAMANI YA GARI AMBAYO IMEFANYAKO (USED CARS)

 Vitu ambazo zimesaa fanyakazi, kimataifa hazina thamani kwa-ajili ya utafauti  ambayo inatoka kwa upungufu wa uwezo (wear and tear) na kwa hivyo URA imeweka msingi wa data (data base) za magari ambazo zimesaa-fanyakazi, ambazo zinamaanisha thamani ya forodha (customs value) ya magari ambazo zimesaa-fanyakazi tayari, zimesaa-amuliwa.

 Pahali pa msingi wa data (database) ya thamani ya magari ambazo zimesaa-fanyakazi kwasababu ya kupima thamani ya magari ambazo zimesaa-fanyakazi na kutofanyisha bei ambayo iko kwa ankara (invoice) namna ya mashauri ambazo zimepeyana na Amri ya EAC kwa kupima thamana ya bidhaa ambazo zimesaa-fanyakazi ya 13 Desemba 2013. Pahali pa msingi wa data (database) ya kupima Thamani ya magari ambazo zimesaa-fanyakazi (data base) ziko kwa tovuti ya URA http://ura.go.ug, chini cha maada ya Kodi ya A-Z.

 Ya nauli/kodi ya mazingira

SN

Aina ya gari

Chini cha miaka 9

Miaka  9 -15

Zaidi ya miaka 15

1

Gari ya abiria/ gari la saluni

         —

 50%

Hairuhusiwi

2a

Gari ya kubeba mzigo ya jumla la uzito wa chini cha kilo 4,000

         — 

 20%

Hairuhusiwi

b

Gari la kubeba mzigo ya jumla ya uzito wa 4,000 na zaidi.

         —

20%

Hairuhusiwi

3

Pikipiki

         —-

20%

Hairuhusiwi

 

 Sio kwenye mabano (NB)

 URA inapeyana kikokotoo (calculator) ya kusaidia kwa kurahisisha hesabu ya kodi ya gari. Inaweza kutumika kwa tovuti ya URA, https://ura.go.ug, chini cha chombo (tool) cha kodi>>kokokotoo calculator (kikokotoo) ya hesabu ya gari.

TAHADHARI

 Habari hii ni ya kipekee ya kutoa ushauri, kwa wateja wetu na kwa wakati wowote kuna uwezo wa  kufanyiwa marekebisho ya kisheria cha kodi na masharti zote za utawala wa kodi.

Add to Bookmarks
Print Friendly, PDF & Email
(Visited 100 times, 1 visits today)
Add to Bookmarks (0)
Print Friendly, PDF & Email

No Comments yet!

Your Email address will not be published.

Skip to content